Wakati ndoa nyingi zikifungwa na kuvunjika muda mfupi baadaye duniani,sio hivyo kwa Herbert na Zelmyra Fisher wa James City N.C. Zelmyra na Herbert Fisher wameoana tangu 13 May 1924. Herbert na Zelmyra Fisher wanasema kwamba siri ya ndoa yao kukaa sana ni Mungu na Kanisa Continue reading
Orodha kamili ya mabilionea na matajiri wakubwa ishirini (20) duniani 2011 hii hapa: Tajiri na bilionea wa kwanza duniani Carlos Slim Helu wa Mexico Tajiri na bilionea wa pili duniani Bill Gates wa Marekani Tajiri na bilionea wa tatu duniani Bernad Arnault wa Ufaransa Tajiri na bilionea wa nne duniani Warren Buffett wa Marekani Tajiri na bilionea wa tano duniani Larry Ellison wa Marekani Continue reading
Mnyama Mwenye Mdomo Mkubwa Kuliko Wote Duniani ni Kiboko. Kiboko ndiye mpaka sasa hivi anayeongoza duniani kwa kuwa na mdomo mkubwa. Pia anaongozo kwa kupanua mdomo anapopiga miayo. Mdomo wake unaweza kupanuka mpaka digrii 170 ambayo ni sawa na mstari ulionyooka ukipungua kwa digrii kumi (10) tu. Continue reading
Tembo wa Afrika ndiye mnyama wa nchi kavu mkubwa kuliko wote duniani. Tembo wanapatikana kwa wingi katika mbuga za wanyama za Tarangire, Ngorongoro, Serengeti, Ruaha, Mikumi, nk. nchini Tanzania Continue reading

Ehud Barak-Waziri wa Ulinzi wa IsraelMatamshi aliyoyatoa waziri wa ulinzi wa Israel, Ehud Barak alipokuwa akihojiwa na mtangazaji Ayala Hasson wa Kituo cha redio cha
Israeli yaleta mgawanyiko na hasira Tanzania. Kimsingi yalimaanisha Tanzania “Haina umuhimu wowote kwa Israel. kama ilivyo Ujerumani, Ufaransa na Uingereza

Nukuu: “Germany, France and England are not Tanzania, Mauritania or Tripolitania [jimbo mojawapo nchini Libya],”….

Alieleza Ehud na… Continue reading

Nchi 20 zinazoongoza duniani kupokea misaada ya kimaendeleo ni Iraq (Dola Bilioni 9.115) ikifuatiwa na Afghanistan (dola bilioni 3.951. Nchi ya Tanzania ni ya tatu kwa kupokea dola takribani bilioni 2.811 kwa mwaka

Nchi zingine ni hizi hapa chini

NCHI

MSAADA KATIKA

BILIONI ZA DOLA

1.  IRAQ

9.115

2.    AFGHANISTAN

3.951

3.    TANZANIA

2.811

      4.    VIETNAM… Continue reading

Je wajua historia ya tajiri wa pili duniani Warren Buffet? Yeye anamiliki zaidi ya dola za kimarekani bilioni 50 na ameshachangia zaidi ya billion 30. Haya ndio baadhi ya mambo yake muhimu kuzingatia:

  1. Alinunua shea za kwanza akiwa na miaka 11 tu. Sasa anajuta kuwa alichelewa kununua shea
  2. Alinunua kashamba kadogo akiwa na miaka 14 tu kwa fedha alizodunduliza kwa… Continue reading

Je Wajua kwamba ROSTAM AZIZ Ajivua gamba CCM kupitia hotuba yake aliyoitoa mbele ya wazee na wanachama wa CCM Igunga. Fuatilia hotuba yenyewe hapa chini:
UTANGULIZI

WAZEE wangu, kwanza kabisa kabla ya kueleza kile ambacho kimenisukuma kuzungumza nanyi leo, napenda kuanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kufikia siku hii ambayo inatukutanisha waja wake.

Wazee wangu wa… Continue reading

Osama Bin Laden – Gaidi Mkubwa Kutokea Duniani Amekufa

 

 

Gaidi mkubwa kabisa kutokea duniani Osama Bin Laden amekufa baada ya shambulizi la kushtukiza lililofanywa na majeshi ya kimarekani katika nyumba yake ya ghorofa tatu. Taarifa za kiitelijensia zilisema kwamba Osama alikuwa akiishi katika ghorofa ya tatu ya ghorofa hiyo. Taarifa hiyo ni ya kweli na hayo yalidhibitishwa baada… Continue reading

 

 

Wamarekani wengi washeherekea kifo cha Osama huku wakighubikwa na kumbukumbu za vifo vya wapendwa wao
Wamarekaani wengi wamekuwa wakishereherekea kifo cha Osama katika viwanja vya ground zero, Newyork huku wakikumbuka orodha ndefu ya wapendwa wao waliopoteza maisha World Trade Center Septemba / 11 na baada ya hapo katika maeneo mbalimbali duniani kwa sababu ya OSAMA BIN LADENI

Timu ya soka bora duniani mwaka 2011kwa viwango vya FIFA (SHirikisho la Soka Duniani) ni timu ya Taifa la Hispania, Timu za Greece, Norway, Urusi, Italy, Chile, Ghana, Slovenia, Japan zimepanda viwango vya kandanda, timu ya ufaransa imeshuka kiwango cha soka kwa viwango vya FIFA.

Timu zingine 20 bora duniani hizi hapa:-

  1. Hispania 18870
  2. Uholanzi 17230… Continue reading

Je wajua kuwa nchi ya Sudani ya Kusini itakuwa nchi ya kwanza mpya duniani kwa mwaka 2011? Hayo yatatimia baada ya wasudani 98.8% raia wa Sudan ya Kusini walioko ndani na nje ya Sudani ya kusini kupigia ndiyo kwa kura ya maoni ya je Sudani ya kusini ijitenge au la. Tarehe 1 Julai 2011 ni siku muhimu kwa nchi inayodhaniwa… Continue reading

CHAMA TAWALA CHA TUNISIA CHA RCD CHAPIGWA STOPTaarifa kutoka Tunisia zinasema kuwa serikali ya mpito ya Tunisia kupitia kwa waziri wa mambo ya ndani imesimamisha shughuli zote za kilichokuwa chama tawala kilichokuwa kikiongozwa na aliyekuwa Raisi wa Tunisia aliyekimbilia Saudi Arabia, Zine El Abidine Ben Ali. Hatua hiyo ilifikiwa huku ikiosubiri maamuzi ya kikatiba ya kukiua kabisa chama hicho kikongwe cha Tunisia cha RCD ili kupunguza kudidimia… Continue reading

Baba mdogo kuliko wote duniani huyu hapa na mke wake

Mtoto Face Alfie, ambaye ana miaka 13 (kulia)ndie baba mdogo kuliko wote duniani. Yeye pamoja na rafiki yake wa kike Chantelle Steadman (15) (kushoto) kutoka Sussex County nchini Uingereza waliamua kumzaa Maisie Roxanne mwenye ratili 7  katikati

Chanzo chetu: The Sun

harusi ghali kuliko zote duniani
Harusi ya kwanza kwa ughali duniani – Vanisha Mittal, na Amit Bhatia iliyogharimu milioni 78 dola za kimarekani

Katika taarifa yetu hii tutaangalia vitu muhimu katika harusi kama vile Aina na idadi ya waalikwa, chakula, keki, gauni la bibi harusi, vifaa vya muziki na mapambo nk. Kwa matajiri mabilionea mara zote hutawaliwa na manukato ya gharama, walikwa wenye majina, watumbuizaji… Continue reading

Kiumbe mkubwa kuliko wote duniani

Nyangumi wa bluu ndie kiumbe mkubwa kuliko wote duniani. Ameripotiwa kufikia mpaka urefu wa futi 110 na uzito wa tani 209

Mmiliki wa kampuni mdogo kuliko wote duniani ni Suhas Gopinath wa India

Akiwa na miaka 14, miaka 10 iliyopita alianzisha Globals Inc ambayo ni kafteria ya internet huko Bengaluru, India hakujua kuwa yeye ndiye mmiliki wa kampuni mdogo kuliko wote duniani

Leo hii  Globals ni kampuni kubwa ya mamilioni ya dola za kimarekani yenye ofisi zake nchini  Marekani, India, Kanada,… Continue reading

Duma anayepatikana Afrika ndiye kiumbe wa nchi kavu anayekimbia kuliko wote duniani

Duma anaweza kukimbia mpaka kilomita 113 kwa saa na anaweza kuongeza mwendo kasi kutoka kilomita 0 mpaka 70 kwa saa kwa sekunde 2

Mbuni anayepatikana Africa ndiye ndege mrefu kuliko wote duniani na anakadiriwa kufikia urefu wa futi 9 na uzito wa kilo 156

Kwa maelezo zaidi bonyeza hapa…

Chatu wa mashariki mwa asia na india ndiye nyoka mrefu kuliko wote duniani na ameripotiwa kufukia urefu wa futi 32.

Kwa maelezo zaidi bonyeza hapa…

Jiunge Kupokea Taarifa

Weka barua pepe yako hapa kupokea taarifa mpya zinapotokea


 

RSS News

Waliotutembelea

Waliotutembelea Leo: 67
Jana: 55
Mwezi huu: 1773
Jumla: 14319
Walioko hewani Sasa: 2
Waliosoma leo: 1922
Waliosoma jana: 1755
Mwezi huu: 35931
Jumla: 88456